Saturday, 30 June 2012

Qur'an Na Maisha Ya Mbu (Mosquito)


Qur’an inatuhimiza kufanya uchunguzi wa viumbe mbalimbali, ili tupate kuona, kujua na kuelewa kwa kina mazingira yetu. Ili tupate kumjua vizuri Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala). Kuwepo kwa viumbe hai na visivyo hai ni moja ya mazingatio makubwa sana kwetu sisi wanadamu, kama tutakuwa ni watu wa kutafakari kwa kina.

Na tutapoweza kuchunguza hapo ndipo tutakapoweza kuujua utukufu wa Mwenyezi Mungu  (Subhaanahu wa Ta’ala). Mwanadamu ana wajibu mkubwa kabisa kuujua ulimwengu wake na vinavyo mzunguka. Qur’an 45:4 Allah (Subhaanahu wa Ta’ala) anatuambia hivi...

Na katika umbo lenu na katika wanyama alio watawanya zimo Ishara kwa watu wenye yakini. 
Qur’an Surat Al-Jaathiya (45):04

Viumbe vyote vinavyo tuzunguka, vinaashiria kuwepo kwake Allah (Subhaanahu wa Ta’ala), na haya ni kwa yule tu mwenye Akili yenye kutafakari kwa kina na mwenye kutafuta sababu za kuwepo vitu hivyo. Qur’an imetaja baadhi ya viumbe hai na visivyo hai, wakiwemo wanyama na wadudu. Na mmoja kati ya wadudu waliotajwa ndani ya Qur'an ni mdudu Mbu.

Hakika Mwenyezi Mungu haoni haya kutoa mfano hata wa mbu na ulio wa zaidi yake. Ama wale walio amini hujua ya kwamba hiyo ni haki iliyo toka kwa Mola wao Mlezi, lakini wale walio kufuru husema: Ni nini analo kusudia Mwenyezi Mungu kwa mfano huu? Kwa mfano huu huwapoteza wengi na huwaongoa wengi; lakini hawapotezi ila wale wapotovu” 
Surat Al-Baqara (2): 026

Wengi humuona Mbu kama kiumbe wa kawaida tu, asiye na mazingatio yoyote yale, zaidi ya kuwa ni mdudu msumbufu na mweye kuleta maradhi (Homa ya kidingapopo au Homa ya uti wa Mgongo, (dengue), Homa ya mto Nile (west Nile virus), Malaria, Homa ya Matende na Mabusha, Homa ya Manjano n.k).

Lakini Mwenyezi Mungu (Subhaanahu wa Ta’ala) amemtaja ndani ya kitabu chake cha Qur’an? Basi hebu tumwangalie mdudu huyu ana nini zaidi ya kuleta maradhi?

MAISHA YA MBU

Kuna aina zipato  3,500 za Mbu duniani zimekwisha gunduliwa mpaka sasa. Lakini wengi wetu tunajuwa aina mbili mpaka tatu za Mbu, ambao ni Anofelesi (Anopheles), Kyules (Culex) aina nyingine ni Kuliseta (Culiseta) na Aidesi (Aedes).

Kama ilivyozoeleka kuwa Mbu ni mnyonya damu (blood sucker), na anaishi kwa kutegemea damu. Japokuwa ili si sahihi sana, kwani si Mbu wote wenye kutegemea damu, ili waishi. Mbu anayenyonya damu ni mbu jike tu, na tena ni kwa sababu ya kutaka kurutubisha mayai yake, kwani kwenye damu ya binadamu au mnyama kunapatikana protin na virutubisho vingi. Mbu dume yeye utegemea nekta au ute na majimaji yanayopatikana kwenye mimea mbalimbali.


Aedes:

Mbu aina ya Aidesi usababisha maumizi anauma mtu, usababisha uchungu na maumivi yenye kusumbua sana, na mara nyingi kushambulia wakati wa mchana (si wakati wa usiku). Aina hii ya Mbu hawana tabia ya kuingia majumbani au kwenye makazi ya watu, na wanapendelea sana damu za Wanyama na binadamu. Mbu awa ndio wenye kuasmbaza Homa ya Uti wa Mgongo na Homa ya manjano.

Mbu awa wana uwezo wa kuruka na kwenda kutafuta mawindo yao masafa marefu sana kutoka kwenye mazalia yao

Culex:

Kyules ni Mbu msumbufu pia, kama alivyo Aidesi, tofauti yake Mbu huyu hupendelea kushambulia wakati wa machweo na baada ya kuingia giza, Kyules tofauti na Aidesi, huyu uingia majumbani kwa ajili ya kujitafutia chakula ambacho ni damu ya binadamu.

Vilevile unyonya damu za viumbe wengine kama vile Ndege wanaofugwa na wasiofugwa. Lakini mara zote wanapendelea damu ya Binadam, na mifugo kama vile ng'ombe, Punda au farasi. Kyules anajulikana sana kwa kusambaza ugonjwa wa malale (encephalitis), Mbu huyu anauwezo wa kuruka mpaka umbali wa kilomita mbili kutoka kwenye mazalia yao. Na wanaishi umri wa wiki chache tu wakati wa miezi ya majira ya joto.


Anopheles:
Ndio Mbu pekee anaye eneza ugojwa wa malaria kwa binadamu.


Culiseta:

Mbu huyu usumbuwa sana kipindi cha mchana na hata jioni, na haswa kama unapendelea kupumzika kwenye vivuli vya miti.

Cha kuzingatia hapa, mbu tunayemuona mara kwa mara ni majumbani mwetu ni mbu jike. Kwa sababu ni mbu pekee anayehitaji joto na kuwa karibu na binadamu ili apate mlo wake wa kurutubisha mayai tumboni.

Mbu huvutiwa na vitu vya aina nne, kwanza mbu huvutiwa na joto, pili mbu huvutiwa na harufu ya mwili (body odor), tatu mbu huvutiwa na kaboni monoskaid (carbon monoxide, co), na Mwisho huvutiwa na mwanga (Light).

Mbu wote kwa kawaida huhitaji maji yaliyotuama (stagnant /standing water) ili kuweza kutaga mayai yake. Maisha ya mbu yamegawanyika sehemu zipatazo nne yaani mayai (eggs), kiluwiluwi (larvae), Buu (pupa) na Mbu aliye kamili (adult).

Mbu jike uhitaji damu ili aweze kurutubisha na kuyapa lishe bora mayai yaliyoko tumboni mwake. Hali ni tofauti kwa Mbu dume yeye hahitaji damu ili aishi, Mbu dume yeye ujilisha kutokana na ute unaopatikana kwenye miti yaani plant nectar.

Mbu jike ana uwezo wa kutaga mayai zaidi ya mia tatu, na huyataga kwa mafungu mafungu kwenye maji yaliyotuama, iwe ni kijito au vidimbwi. Na mara nyingi mayai ya mbu uwa yameungana pamoja, na kuelea juu ya maji. Mayai ya mbu huanguliwa katika kipindi cha saa 24-48 na hii ni kama hali inaruhusu, na baada ya siku 7-10 ndipo Mbu kamili utokea. Na kama ikitokea kuwa hali hairuhusu basi mayai ya mbu yana uwezo wa kuhimili shida na tabu na kuishi bila kutotolewa kwa kipindi cha miaka mingi.

Baada ya kutotolewa kinachotoka hapo huitwa v/kiluwiluwi na hawa viluwiluwi wa mbu ujilisha vijiumbe vidogovidogo vinavyopatikana kwenye maji (micro organisms and organic material).

Mbu kwa kawaida huishi kati ya wiki nne mpaka nane na si wiki moja kama watu wengi wanavyo fahamu. Mayai ya Mbu yanapo tagwa uwa katika rangi nyeupe, na baada ya muda mfupi ufifia na kuwa na rangi nyeusi, ili kuyakinga na maadui wanaokula mayai ya mbu kama vile ndege n.k. Kitu cha ajabu ni kwamba mayai ya Mbu licha ya kuwa na uwezo wa kuisha miaka mingi bila ya kutotolewa, pia yana uwezo wa kuimili baridi kali kabisa kwa kiwango cha digrii chini ya sifuri –0 oc yaani hata kile kipindi cha theruji (winter).

Viluwiluwi vya Mbu pia hubadilika rangi kulingana na mazingira ili kujilinda na maadui. 
Viluwiluwi hutumia vijibomba vidogovidogo vilivyoko kichwani kwa ajili ya uvutaji wa hewa kutoka nje.
Vijibomba ivi vinalindwa na ute maalumu uitwao viscous secretion na kazi yake ni kuhakikisha kuwa hewa inayo vutwa na kiluwiluwi haichanganyiki na maji.

Mbu anapofikia wakati wa kutaka kutoka majini, zile bomba ambazo uzitumia kwa ajili ya uvutaji wa hewa hujifunga. Hali hii utokea pale anapofikia kuwa buu au pupa. Na hali hii huchukua siku tatu mpaka nne katika hali ya kuwa pupa. Na huja juu ya maji katika hali ya kifukofuko (cocoon). Na hapa ndipo mabadiliko ya mwisho kuelekea Mbu kamili utokea.

Kipindi hiki ndio kipindi cha hatari sana kwa Mbu kwani kosa kidogo tu la kiutendaji basi litasababisha kifo chake, kwani hapa hayatakiwi maji kuingia katika gamba la kifukofuko hiki. Lakini kwa uwezo aliopewa, Mbu hutoka hali ya kuwa yu wima nje ya maji, na anakuwa hana uwezo tena wa kuzama ndani maji. Na kama ikitokea kuwa atazama ndani ya maji hii itasababisha uhai wake kutoweka na kufa kabisa.

Mbu aliye kamili ni mwepesi kuhisi hali ya joto kwa kiwango cha kushangaza kabisa, mbu ana uwezo wa kuhisi joto kwa kiwango cha 1/1000   oC. Mbu anakadiriwa kuwa na macho zaidi ya mia moja (100).

Mbu mara nyigi uwa hategemei mwanga ili aone mawindo yake. Kwani ana uwezo wa kunusa na kuhisi joto la mwanadamu akiwa umbali wa futi 18 kutoka windo lake Lilipo. Vile vile anao uwezo wa kuona mishipa midogo midogo ya damu katika mwili wa mwanadamu hata kwenye kiza kinene.

Mbu anapo tua kwenye windo lake hutumia bomba lililo hifadhiwa katika ala maalumu mbele ya kichwa chake angalia picha hapa chini:

Kichwa cha Mbu

Mbu kwa kawaida uwa hatoboi tundu ili kupata damu kutoka katika mwili wa mwanadamu, au kama vile sindano inavyo ingia mwilini mwa mwanadamu, anachokifanya yeye ni kutumia mdomo wake wenye meno kama msumeno kukata ile shemu anayotaka kupitisha bomba lake kwa ajili ya kunyonya damu. Lakini mwili wa mwanadamu umeumbwa na uwezo mkubwa wa kujilinda kwani damu kidogo tu iwe kwa kujikwaruza ama kujikata inapotoka mwilini huganda, lakini cha ajabu ni kwamba Mbu wanapo uma damu uwa haigandi! Hii inasababishwa na nini? Jibu lake ni rahisi mno, mbu baada ya kukata eneo ambalo anakusudia kupanyonya, upatemea ute maalumu (anti-coagulants) sehemu hiyo ili kuzuiya damu itakayotoka hapo isigande ili yeye aendelee kunyonya damu raha mustarehe.

Baada ya Mbu kumaliza shida zake na kuondoka ndipo na sisi uhisi zile shemu tulizoumwa na mbu zikiwasha. Hii inasababishwa na ule ute alio utumia Mbu wakati wa kunyonya damu. Sasa hapa kuna maswali ya kujiuliza.

  • · Kwa jinsi gani Mbu ameweza kugundua kuwa mwanadamu ana enzyme inayomsaidia kugandisha damu wakati inapotoka na kukutana na hewa ya nje?
  • · Pili ni kwa jinsi gani Mbu ameweza kutengeneza ute (anti-coagulants) ambao akiutumia basi usababisha damu itokayo mwilini mwa mwanadamu isigande?
  • ·  Tatu utaalamu huo wa kutengeneza u anti-coagulants amejifunza wakati gani na kwenye maabara gani?
Kwa sisi Waislamu jibu lake ni rahisi sana. Kwani tunaamini kuwa hivyo ndivyo alivyo umbwa na Mola wake Allah (Subhaanahu wa Ta’ala).

Yeye ndiye Mwenyezi Mungu, Muumbaji, Mtengenezaji, Mtia sura, Mwenye majina mazuri kabisa. Kila kilioko katika mbingu na ardhi kinamtakasa, naye ni Mwenye kushinda, Mwenye hikima
Qur’an Surat Al-H'ashri (59): 24

Kinamsabihi kumtakasa Mwenyezi Mungu kila kiliomo ndani ya mbingu na ardhi. Na Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima. Yeye ndiye Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi. Anahuisha na anafisha. Na Yeye ni Mwenye uweza wa kila kitu. Yeye ndiye wa Mwanzo na ndiye wa Mwisho, naye ndiye wa Dhaahiri na wa Siri, naye ndiye Mjuzi wa kila kitu.
Qur’an Surat Al-H'Adiid (57):1-3

Mbu aliye kamili ni mwepesi kuhisi hali ya joto kwa kiwango cha kushangaza kabisa, mbu ana uwezo wa kuhisi joto kwa kiwango cha 1/1000 centigrade . Mbu anakadiriwa kuwa na macho zaidi ya mia moja (100).

Mbu mara nyigi uwa hategemei mwanga ili aone mawindo yake. Kwani ana uwezo wa kunusa na kuhisi joto la mwanadamu akiwa umbali wa futi 18 kutoka windo lake Lilipo. Vile vile anao uwezo wa kuona mishipa midogo midogo ya damu katika mwili wa mwanadamu hata kwenye kiza kinene.

Mbu anapo tua kwenye windo lake hutumia bomba lililo hifadhiwa katika ala maalumu mbele ya kichwa chake angalia picha hapa chini:


Je, unajua?
Je, unajua ukweli wa mambo yafuatayo Kuhusiana na mbu?

1.      Kuna aina zipatazo 3500 za Mbu Duniani, lakini wengi wetu tunajuwa aina mbili tu za Mbu, Culex na Anopheles basi
2.      Mbu uzito wa milligrams kati ya 2 na 2.5
3.      Mbu jike wanaweza kunywa karibu lita 5/1000000 ya damu kwa siku (Aedes aegypti)
4.      Kuna uwezekano ni mkubwa sana wa kuumwa na Mbu kama wewe ni mlaji wa ndizi
5.      Wakati wa mwezi mwangaza, (full moon) ongezeko la watu wanao umwa na Mbu uongezeka mara 500 na zaidi.
6.      Mbawa za Mbu upiga mara 500 kwa sekunde.
7.      Ugonjwa unao ongoza kwa kuuwa ni ugonjwa unao sababishwa na Mbu wa Marilia aitwaye Anopheles 
8.      NI ukweli kwamba Mbu wanapendelea kuuma watoto wadogo kuliko watu wazima
9.      Mbu wanachukia na hawapendi harufu inayotoka kwenye Mchaichai, inaumiza miguu yao.
10.  Mbu wana uwezo wa kuhisi na kunusa windo lake kwa umbali wa Mita 20 mpaka 35
11.  Mbu dume anaweza kuishi kati ya siku 10 na 20
12.  Mbu jike anauwezo wa kuishi kati ya siku 3 na siku 10

Tuesday, 19 June 2012

Qur'an Na Maisha Ya Mdudu Chungu [AnNam’l] Ant

Hebu fikiria kuwa umefika kwenye jengo la kijeshi, jengo ambalo ndio makao makuu ya jeshi la nchi fulani. Bila shaka  jengo ilo litakuwa ni jengo lenye kulindwa kwa ulinzi wa hali ya juu sana. Walinzi walio katika mageti ya kuingia ndani ya jengo ilo wapo makini na kazi yao, wanaofuata amri kikamilifu sana. Vilevile jengo ilo linalindwa na mitambo ya hali ya juu sana. Hii yote ni kumzuia mtu au adui yeyote asiyetakiwa kuingia hasiweze kuingia ndani.

Tuchulie wewe umeweza kuingia ndani, japo kibahati, na humo ndani ukakuta maelfu ya  askari wakifanya shughuli zao kwa ukakamavu wa hali ya juu sana, na askari hao wanafuata amri bila ya kusita. Jambo ili lina kustaajabisha kidogo, na unaanza ujiuliza nini siri yake.

Muda kidogo unagundua kuwa, jengo ili limejengwa katika hali ambayo inampa nafasi kila askari, kufanya kazi zake bila tatizo lolote na bila usumbufu wa hali yoyote, kwani katika jengo ilo kuna idara mbalimbali kwa kazi tofauti tofauti, katika jengo ilo kuna majengo ya chini ya ardhi, lakini cha kushangaza hewa inaweza kufika bila matatizo yoyote yale.

Maghala ya chakula ni makubwa na yamejengwa katikati ya jengo, kiasi ambacho kila askari inakuwa ni rahisi kwake kufika hapo bila ya usumbufu wowote. Lakini kitu kingine cha kushangaza ni kuwa hali ya joto na hewa inayopatikana katika jengo ilo ni sawasawa. Uwe chini au juu ya ardhi hali ni ileile tu. Unagundua kuwa kumbe kuna mfumo (system) wa uingizaji na utoaji wa hewa ndani ya ilo jengo. Mfumo ambayo unafanya kazi kiasi ambacho inakushangaza hata wewe, kwani mfumo huyo una saidia kuweka hali ya joto isizidi wala kupungua katika siku zote za mwaka mzima.

Yaani ukiwa umo ndani huwezi kuhisi kama hivi sasa ni kipindi cha joto ama baridi, kiasi ya kwamba mtu akikuuliza hivi, “Ili jengo ni mhandisi gani aliye lijenga?” Jibu lake litakuwa “Mhandisi aliye jenga jengo ili bila shaka ni mhandisi mahiri sana, na watu waliye msaidia ni watu wenye ujuzi na elimu ya ujenzi wa hali ya juu sana. Na wenye akili na utamaduni wa kujenga majengo ya aina hii.”

Lakini jambo la kushangaza jengo ilo unalolisifia kuwa limejengwa na mtaalam/wataalamu wenye ujuzi wa hali ya juu sana, wataala hao si wengine ila ni wadudu. Wadudu ambao kwa umoja wao wanapozaliwa /wanapotoka tu kwenye mayai yao wanajua wajibu wao bila ya kuelekezwa na bila ya kupoteza muda. Hii inaonyesha kuwa wadudu hawa wanapata ujuzi huu kabla ya kutoka katika mayai yao. Swali “Je ni wadudu gani hao? Na nani huyo aliye wafundisha hayo yote? Hao si wadudu wengine zaidi ya jamii ya Mdudu Chungu (Ants).

Kabla ya yote kwanza inatupasa tumwelewe mdudu Chungu ni mdudu wa namna gani.
 Kamusi ya kiswahili sanifu hiliyotolewa na TUKI ya mwaka 1981 inaeleza maana ya Chungu katika fungu  [D] (ji) kuwa ni mdudu mdogo mweusi wa jamii moja ya Mchwa, Siafu, Sisimizi, Nyenyere, Majimoto au Koyokoyo. Kwenye kijarida iki tutaeleza maelezo ya jumla kuhusu wadudu hawa. Ambao wameumbwa wakiwa na magamba magumu (exoskeleton), kiasi ukiwakanyaga uvunjika vunjika.

A: Mawasiliano ya Mdudu Chungu:
 Qur’an inatuelezea habari ya kushangaza kidogo pale tunapomsoma nabii  Sulaiman na jeshi lake walipokuwa wakipita katika bonde la Chungu.    
(Surat An-Naml 27:18-19). Kuwa …

“Mpaka walipo fika kwenye bonde la wadudu chungu, alisema mdudu chungu mmoja: Enyi wadudu chungu! Ingieni majumbani mwenu, asikupondeni Sulaiman na majeshi yake bila ya wao kutambua…” 
Qur’an 27:18-19

Je akili yako na yangu inakubaliana kweli na ili jambo? Yawezekana tukaamini tu kwa sababu ya imani zetu kwa Mwenyezi Mungu. Lakini kama tukiondoa imani tulizo kuwa nazo, na kutumia elimu zetu za kawaida je  Mdudu Chungu na jamii zake kwa ujumla, (Koyokoyo (majimoto) Mchwa, siafu, sisimizi au Nyenyere n.k), wanaongea au wanawasiliana na kuelewana kwa kila jambo wanalo lifanya kwa Lugha yao? Kabla ya kufika uko na tuangalie nini maana ya kuwasiliana na nini maana ya Lugha. Kamusi ya Kiswahili sanifu iliyotolewa na TUKI ya mwaka 1981 uk, wa 145-146 inasema hivi...

1. Lugha ni mpangilio wa sauti na maneno unaoleta maana ambao hutumiwa na watu wa Taifa au kabila Fulani kwa ajili ya kuwasiliana*.
2. Lugha ni maneno na matumizi yake.
3. Lugha ni maneno anayotumia mtu kujieleza.

Vile vile hapa kuna maneno haya, ... mpangilio wa sauti.

Ni nini maana ya sauti?
Sauti ni Dhati ya chochote kinachoweza kusikika kutokana na mgongano au msuguano wa vitu kama vile mlio au usemi n.k.

Bado kuna maswali hapa ni nini mlio? 
Mlio ni sauti inayotoka wakati vitu vinapogongana, kugusana, kukwaruzana, au kufyatuka au ni sauti anayotoa mnyama au wadudu wakati wanapolia.

Je nini maana ya *wasiliana?
Wasiliana ni kupashana habari au taaarifa au ujumbe.

Baada ya kufahamu hayo basi inabidi tufahamu aina za mawasiliano, je kuna aina ngapi za kuwasiliana? Kwenye lugha kuna mawasiliano ya aina nyingi, lakini zilizo zoeleka ni hizi zifuatazohapa chini:

1. kuwasiliana kwa Sauti. (ni haya maneno tunayotamka kila siku).
2. kuwasiliana kwa kutumia Alama. (kama vile alama za barabarani nk).
3. kuwasiliana kwa kutumia Vitendo. (kama vile wanavyo wasiliana viziwi nk)
4. kuwasiliana kwa kutumia Harufu. (Pheromones) (kama vile wanavyo wasiliana wadudu au wanyama kwa kutaka kujua siku zao za kupandwa mf; mbuzi nk.

kwa hali hii basi tunaona kuwa mawasiliano yapo ya aina mbalimbali, tatizo tu ni kuwa je lugha inayotumika au mtindo unaotumiwa kuwasiliana tunauelewa au kuufahamu? Je sauti tunazozisikia au vitendo na harufu zinazotolewa na viumbe mbalimbali tunazielewa na kuzitambua? Inawezekana kuwa sauti au harufu unayoisikia unaifahamu kuwa ni ya kiumbe fulani, lakini je unaelewa ina maana gani? Basi na tuangalie watafiti wa karne hii wanalionaje suala ili.

Tafiti za kisayansi za karne hizi tulizo nazo, zimethibitisha hayo kuwa kuna mawasiliano ya hali ya juu sana katika jamii hizi za Chungu yaani kwa  kingereza wanasema “There is an incredible communication network among these creature.” Chungu ambao tunawaona ni wadudu wanaotumia milango ya fahamu kupitia Antenna, antenna ambazo hufanya kazi kama zifanyavyo kazi Pua kwa kunusa, na kama vifanyavyo vidole kwa kushika, na vilevile midomo kwa kuonja ladha mbalimbali, wadudu hawa pia wana vinyweleo vidogo vidogo sana ambavyo huwasaidia kuhisi kitu chochote kinacho wagusa.

Wadudu hawa wenye ukubwa usiozidi milimita 2-3, wana nervecells zipatazo nusu milioni yani 500,000. Ambazo zimekusanywa katika mwili wenye mm 2- 3  tu. Wadudu hawa wenye uwezo wa kutoa sauti ndogo ndogo wana uwezo wa kufanya mawasiliano miongoni mwao, kwa kutumia harufu (Odor), maji maji na  kugusana  kwa kutumia antenna zao, kiasi ambacho imefanya iwe rahisi kwao katika kutafuta mawindo, kujenga viota vyao, kupigana vita na kufanya harakati mbalimbali za kila siku, hata kuwashinda viumbe wengine wenye akili kama binadamu. Kwani  katika maisha yao hawana kitu kinachoitwa ubinafsi au choyo.

Mawasiliano na maelewano miongoni mwao ni makubwa sana kwa asilimia mia moja (100%) zaidi kuliko yale ya binadamu, ambayo yamejaa ubishi, maswali, na kutokuwajibika. Kiasi ambacho mpaka tunajenga choyo,ushabiki na ubinafsi wa hali ya juu sana.

B: Upatanishaji Habari:
Mdudu Chungu anapopata  eneo jipya la kuishi au anapopata windo jipya, huwafahamisha wenzie kwa kutumia ugiligili. Ugiligili ni ute hutokao katika matezi (glands). Majimaji hayo yanaitwa ‘Pheromones’. Na kama windo ni kubwa au liko mbali, basi kila chungu aliyepata habari ya  windo jipya au eneo jipya la kuishi utoa majimaji hayo, kuelekea uko kwenye windo jipya, ili kila mmoja apate kupafikia kwa urahisi. Maji maji hayo wanayo yatoa yana harufu, harufu ambayo ni wao tu ambao wanaotoka kiota kimoja ndio wanayoifahamu.

Na ikitokea kwamba wanahama toka eneo moja kwenda eneo lingine, basi kila mmoja hujitahidi kuacha alama, ili iwe rahisi kwa mwingine kufuatilia ni wapi wanapaswa kuelekea.

Na wanapo fanikiwa kufika katika kiota kipya, basi kazi ya kila mmoja wao inakuwa kupaka majimaji yao katika kiota hicho kipya. Ikiwa ndio kama alama ya umilikaji wao mpya wa kiota hicho. Katika hali hii ya kuunda makazi mapya hamna hata mdudu mmoja anayekaa tu bila kazi, hapa kila mdudu ni mfanyakazi asiye na msimamizi mfano.

  • Kuna ambao kazi yao ni ulinzi
  • Kuna ambao kazi yao ni kutafiti, wanaangalia mazingira mapya yakoje
  • Kuna  ambao kazi yao ni kukusanya chakula
  • Kuna  ambao kazi yao ni ujenzi.
  • Kuna  ambao kazi yao ni kuangalia watoto n.k

Kwa akika kabisa hatuwezi kulichukulia ili kama ni jambo la bahati nasibu tu, au ni jambo ambao wadudu hawa wamelifanyia mazoezi kwa kipindi kirefu sana. Na hasa katika mgawanyo wao wa kazi za kila siku. Ukizingatia kuwa ile dhana ya Evolution inayosema kuwa kila kiumbe kinajifikiria chenyewe tu ili kiishi (ubinafsi).
(Every creature thought only for his/her own life and interest only to survive. (Survival of the Fittest). 

C: Mawasiliano ya kikemikali (Chemical communication):
Kama tulivyoeleza hapo mwanzo, kuwa sehemu kubwa ya maisha ya wadudu hawa yanategemea sana mawasiliano, mawasiliano ambayo yanatumia majimaji kwa kupitia tezi (Glands) za aina sita, kutegemea na aina ya mdudu. Majimaji haya yanajulikana kama Pheromones na Allomones.

*Allomones ni material inayotumika  kwa Inter-Genus Communication (yaani kwa spishi zinazo fanana mfano, mchwa na mchwa wa kichuguu kingine).
*Pheromone a chemical signal, which is mostly used within a genus.

Yaani hutumika kwa mawasiliano ya wadudu wanaokaa pamoja katika kiota kimoja au katika kichuguu kimoja. Ili neno ni mkusanyiko wa maneno mawili yaani neno Pher lenye maana ya Carrying na neno hormones (homoni) kwa maana hiyo neno Pheromone maana yake ni "hormone carriers". (Kichukua homoni).
*aina za Allomones na Pheromone zipo nyingi sana inategemea na aina ya Mdudu husika.

Watafiti wanaeleza kuwa, kila kundi au aina ya chungu wanatoa kemikali hizi kwa ajili ya matumizi na mahitaji yao ya kila siku, kemikali hizi zinatofautiana kutoka aina moja hadi nyingine. Kama ilivyo ada, elimu hii ya kemia ni elimu inayohitaji ujuzi wa hali ya juu sana, na vilevile kunahitajika kufanya majaribio mengi ya kimaabara na ya muda mrefu. Na uku ukifuata miiko ya kisayansi na kufanya marejeo mengi ya kitafiti, kwa wale wajuzi waliokutangulia. Ili uweze kutoa kitu kitakacho tumika bila ya kuleta madhara kwa watumiaji. Lakini ni kitu cha ajabu kabisa kwa wadudu hawa, wadudu ambao wanapata uwezo wa kutengeneza kemikali, ambazo wao wenyewe haziwadhuru na zinatumika wakati wote bila kwisha, kitu ambacho kwa binadamu si rahisi kufanya. Tena basi huzitumia kemikali hizo punde tu wanapototolewa kutoka kwenye mayai, na bila kupoteza muda.

Aina za Tezi (Endocrine Glands):
Aina hizi za tezi (glands) hufanya kazi tofauti tofauti kulingana na aina ya mdudu Chungu mfano; mdudu Chungu aina ya Sisimizi ni tofauti na mdudu Chungu aina ya Siafu vilevile Siafu ni tofauti na Mchwa, basi hata matumizi ya kemikali zao ni tofauti vile vile.


  • Dufour Glands: Homoni zinazo zalishwa hapa hutumika kwa ajili ya taarifa (Taadhari). Vile vile utumika kutofautisha kati ya mayai ya malkia na wadudu wa kawaida.
  • The Venom Sac: Ili ni zao la formic acid, maji maji haya hutumika kama silaha wakati wa mapambano, pamoja na kujilinda na maadui. Mfano mzuri wa maji maji haya hupatikana kwenye jamii ya Chungu aina ya Fire Ants. Sumu hii inaweza kuwafanya wadudu wadogo wadogo wapooze (paralyze) au hata kufa, na hata pia huweza kusababisha miwasho kwa baadhi ya watu au kuwaletea mzio (Allergy).
  • Pygidial Glands: Aina tatu za Chungu hutumia maji maji haya kama alama ya tahadhari Chungu wanaopatikana majangwani na Amerika ya kusini hutumia maji maji haya yenye harufu kali kama alama ya tahadhari na kujilinda na maadui.
  • Sternal Glands: Maji maji yanayotoka katika tezi hizi hutumika wakati Chungu wanapohama au kufuatilia mawindo (Tracking Prey), na kuwakusanya Askari pamoja. Lakini mara nyingi majimaji haya hutumika sana kwa Chungu kujipaka matumboni mwao ili waweze kuzungusha matumbo yao vizuri wakati wa kuwashambulia adui. Maji maji haya huwasaidia wadudu hawa kuweza kuyachezesha matumbo yao uku na uko kwa urahisi na vilevile huondoa mikazo katika misuli.
  • Metapleural Glands: (metasternal or metathoracic glands) Maji maji haya hutumika kama kinga (Antiseptics), kutokana na wadudu wanaoweza kuwadhuru Chungu katika miili yao au majumba yao wanamoishi, mfano wa dawa inayotoka katika tezi hii ni kutoka kwa Chungu aitwae Atas na dawa anayotoa ujulikana kwa jina la Phenylacetic acid, dawa hii Chungu anaibeba kwa wastani wa uzito wa 1.4 microgram kwa wakati wote. Chungu jamii ya Walker huweza kutoa kinga hii mara tu anapoguswa na mdudu ambaye ni adui.

Kumbuka kuwa wadudu hawa jamii ya Chungu sio kwamba wao ni mahodari sana au wanawajua maadui zao, la hasha ila kinachotokea hapa ni kuwa bila ya wao kutaka wanapo guswa tu na vijiumbe vya maradhi (Microbes), basi miili yao hutoa kinga hii bila kuchelewa au bila ya wao kutaka (involuntarily). 

Wachambuzi wa damu za viumbe hususani za wadudu, wanaeleza kuwa wadudu hawa bila ya kuwa na kemikali hii basi wangekwisha toweka ulimwenguni miaka mingi iliyopita na wasingekuwepo katika uso wa dunia hii. Hali hii inapingana sana na ile dhana ya Evolution, dhana ambayo inaelezea ngazi za kimaendeleo kwa viumbe. Kuwa walianza katika hali duni (Primitiveness) na kuendelea katika maendeleo (Civilization), kutoka hatua moja baada ya nyingine. Hali hii inaonyesha kuwa Chungu kwa kuzingatia Elimu au dhana ya Evolusheni kuwa.

“Ametokana na Nyigu (Wasp). Wadudu hawa, miaka mingi iliyopita hawakuwa wakiishi pamoja na wala hawakuwa na tezi hizi zinazotema kemikali za kujilinda. Sasa kutokana na kuwa na maadui wengi wa aina mbalimbali, basi waliweza kujifunza kujitengenezea dawa (sumu) ambayo wao wenyewe haiwadhuru, bali anayedhurika ni yule ambaye si miongoni mwao. Vilevile kutokana na kuwa na majukumu mengi ya kimaisha, wakaanza kujikusanya na kuishi pamoja, ili iwe rahisi kwao kupigania maisha na kujilinda dhidi ya maadui zao.” ...Huu ni uwongo dhahiri.

Hii ni dhana ambayo haiingii akilini mwa mtu yoyote yule mwenye akili timamu. Rejea Qur’an 31:6-7
Na miongoni mwa watu wapo wanao nunua maneno ya upuuzi, Ili wawapoteze watu Na njia ya Mwenyezi Mungu pasipo kujua, na wanaichukulia ni maskhara. Hao watapata adhabu ya kuwafedhehesha. Na (mtu kama huyo) anapo somewa Aya zetu huzipa mgongo kwa kujivuna, kama kwamba hakuzisikia, kama kwamba masikioni mwake mna uziwi. Basi m’bashirie kuwa atapata adhabu chungu. Qur’an Sulat Luqman 31:6-7

(Kama tulivyo ona kuwa, Qur’an inatuelezea nini kuhusiana na maneno ya upuuzi ambayo watu wengi wenye elimu wanazoziita elimu dunia, wanavyo shadidia mambo mengi ya kipuuzi. Na wala hawafikirii isipokuwa wanachojali ni maslahi yao ya kilimwengu tu).

Basi na turudi katika mada yetu, kitu cha ajabu hapa ni kwamba kemikali zote hizo tulizozitaja hapo juu hutoka bila ya utashi wao, yaani kama vile binadamu anavyo pepesa macho au kama vile mapafu na moyo wa binadamu unavyofanya kazi bila utashi wa mtu yaani involuntarily. Wataalamu wa viumbe hai (Hususani wadudu), wanaeleza kuwa, wadudu hawa hata siku moja hawakuwahi kuishi mmoja mmoja bila ya kushirikiana katika umoja (Colony), kwani katika jamii zao kila mdudu ana kazi yake maalum, bila ya mwingine kuwepo maisha yao hayata wezekana kuwepo. Na ndio maana hivi leo baada ya kugundua DNA wanasayansi wanakubaliana kuwa wadudu hawa walianza kuishi pamoja tangu walipoanza kuwepo hapa duniani, na waliumbwa hivyo hivyo walivyo, tunavyo waona leo hii.

   Na hapana mnyama katika ardhi, wala ndege anayeruka kwa mbawa zake mbili, ila ni umma kama nyinyi. Hatukupuuza kitabuni kitu chochote. Kisha kwa mola wao mlezi watakusanywa.
Qur’an 6:38


D: Utambulisho (The identity card-colony odor):
Kama tulivyoeleza hapo mwanzo kuwa wadudu hawa huweza kutambuana na kuwa tofautisha maadui marafiki au jamaa wanao fanana nao. Hali hii ni tofauti sana na sisi binadamu ambao si rahisi kuwatofautisha wadudu hawa. Hebu na tuangalie ni jinsi gani wadudu hawa huweza kutambuana na wenzao ambao wanatoka kwenye kundi moja au kundi la adui.

Chungu wanapokutana hupapasana kwa kutumia kipapasio (Antenna) zao, ili kuweza kutambuana, kama huyu ni adui, rafiki au ndugu. Hapa utumika ile harufu (odor), ambayo kila jamii (kundi) inatofautiana kutoka jamii moja hadi nyingine.  Mfano; Kama aliyeingia ni wa jamii ileile lakini anatoka kwenye kundi lingine yaani kama ni Mchwa wa kichuguu kingine tofauti, huyu hata shambuliwa, ila watamtambua kuwa ni mgeni, watamkaribisha na atapewa chakula, lakini si kama wenyeji wanaovyokula yeye atapewa lishe kidogo (less food) mpaka pale atapotohoa (adapt) harufu (odor) ya mchwa wenyeji. Harufu yake itakapo fanana na ya wenyeji hapo sasa atapata uraia kamili na atapata haki zote za kupata mlo kamili.

Askari

Kama Mchwa ni wa kundi lile lile basi harufu zao zitafanana na hawata leteana tabu. Kama alieingia ni adui basi atashambuliwa haraka sana, iwe kwa kutumia miba waliyo nayo au kung’atwa na kutumia sumu ya Lormic acid au citronella au sumu nyingine yoyote ile, kutegemeana na aina ya Chungu. Chungu pia hutumia lugha hii ya harufu kama nywira "password", au kitambulisho cha kuingilia katika makazi yao. Kwani kwenye njia za kuingilia katika makazi yao kunakuwa na mlinzi ambaye anafanana na eneo analolinda kwa rangi na muonekano hapa wanatumia mbinu inayoitwa kamafleji (camouflage). Aina hii katika jamii ya Chungu (doorman) wanakuwa si wengi sana, itategemea na idadi ya milango au mipito ya kuingia katika makazi yao.

Majaribio ya kimaabara yameonyesha kuwa Chungu jamii ya fire Ants hutumia aina ya dawa (Pheromones) inayojulikana kwa jina la Haidrokabon (Hydrocarbon) kwa ajili ya kutambuana. Hydrocarbon hii hutumika kupakana wao kwa wao kila wanapokutana, na ikitokea kuwa yule aliyepakwa ni jamii moja lakini anatoka katika kundi lingine, yule aliye mgeni hutaharuki kidogo kwa kuhisi kupakwa kitu ambacho ni kigeni kwake. Lakini kama ni wa kutoka kundi lile lile basi hutulia na kuhisi ni kitu cha kawaida. Harufu hii inayopatikana kutokana na kemikali hii ya Hydrocarbon huwa ina radha tofauti tofauti kulingana na jamii husika. Na kama aliye pakwa dawa hii ni jamii tofauti na wao, basi kutaharuki kwake huwa ni kukubwa sana na uhisi kupakwa kitu hasicho kitambua kabisa, na kuanza kufanya machachali, na hapo atatambulika kuwa huyu aliye ingia ni adui, na atashambuliwa ipasavyo na kutolewa nje.

Wataalamu wa Elimu ya Evolusheni walipoulizwa kuhusu hali hizi za kutambuana wao walieleza kuwa “…hiyo ni hali ya Natural selection yaani ni mabadiliko yanayotokea bila ya kuleta madhara kwa jamii moja inayofanana lakini ikaleta madhara kwa jamii nyingine.”

Lakini cha ajabu wadudu kama vile Nyuki (Bee) anapo mshambulia adui yake humwachia mwiba na kutoa sumu na pia hutoa harufu ya Pheromones inayo tambulisha wenzie kuwa kuna adui au hatari, japokuwa yeye mwenyewe hufa mara tu anapo acha hiyo sumu. Hii inaonyesha kuwa, kemikali hii kwa nyuki hutolewa mara moja tu katika maisha yao. Je mabadiliko ambayo watu wa evolution uyaita Natural selection au Mutation yanapatikana vipi? Je hawa Nyuki mpaka leo hii hawajaweza tu kupata uwezo wa kujitengenezea sumu na miiba isiyo kwisha ili waendelee kuishi na waweze kuvirithisha vizazi vyao vijavyo? Au yupo anaye wajaalia wanapokuwa bado wapo matumboni mwa malkia wao?


Kisha watarudishwa kwa Mwenyezi Mungu, Mola wao wa Haki. Akika, hukumu ni yake. Naye ni mwepesi kuliko wote wanao hisabu.
Qur’an Surat Al-Anaam 6:62


Chungu akibeba Mateka

E: Jinsi ya Kutambuana (kupapasana):
Wadudu hawa aina ya Chungu kama ninavyo endeleakueleza pia wana uwezo wa kutambuana na kutumiana ujumbe kwa kugusana (kupapasana), wadudu hawa wanapokutana hutumia vipapasio (antenna) vyao ili kutambuana. Mmoja hugusa kichwa cha mwenzie juu na chini kwa upole, ili kunusa na kumpaka harufu aliyokuwa nayo ili kujua ana ujumbe gani? Kama ni taarifa ya hatari au kukaribishwa chakula au kutambuana kwa kawaida. Lugha hii ya kutumia antenna huitwa Antennal Language. Lugha nyingine inayotumika katika mawasiliano ni kutoa sauti. Kuna aina  mbili za sauti moja ni ile ambayo mdudu mwenyewe  anaitoa na pili ni ile inayopatikana  kwa kugonga gonga kwenye  kitu kigumu kama vile ubao. Hii ya kugonga gonga mara nyingi hutumika na chungu aina ya Carpenter Ants. Na hii huashiria hali ya hatari, na mara zote wadudu hawa wanapo letewa au kusikia taarifa hii mara moja uelekea kule kunakotokea sauti au mtetemeko wa sauti na mara moja bila kuchelewa huvamia chochote kila wanachokikuta kinatembea. Wadudu Chungu aina ya leaf cutter, hutumia sauti ili kuomba msaada pale wanapo fukiwa kwa bahati mbaya, ili wenzao waje wawatoe.

Chungu Wakipigana

F: Mbinu za kivita na Mateka:
Chungu ni wadudu wa ajabu sana, katika maisha yao mara kwa mara ukutana na upinzani wa aina nyingi sana. Upinzani ambao uwapelekea wao kupigana vita na jamii nyingine iwe Chungu wenzao au wadudu wengine kabisa wasio kuwa jamii ya Chungu. Kuna jamii mojawapo ya Chungu (*Camponotus ants), wao wana uwezo wa kujilipuwa au kujitoa muhanga, kinacho fanyika hapa ni kwamba kama wamevamiwa na adui au na kiumbe yeyote basi wakati wa mapambano baadhi yao huamua kujiua kwa kuvimbisha matumbo yao mpaka wanapasuka, na kusambaza majimaji yaliyo na harufu toka matumboni mwao ambayo huwa ni sumu kwa adui. Kwa jinsi hii anakuwa amejitoa muhanga maisha yake, kwa ajili ya wenzie. Je watu wa elimu ya Evolution theory wana hoja zozote kuhusiana na jambo ili.

Camponotus ants

(Such a serious sacrifice by the ants can not, of course, be explained by either natural selection or by the "evolutionist socialization process").

* Jamii hii ya Chungu imegunduliwa mwaka 1970 na mabingwa wawili wa elimu ya wadudu (entomologist) katika misitu ya Malaysia.

Kuna njia nyingine ambayo ni muhimu sana kwa wadudu hawa katika mapambano yao. Nayo ni ya kutumia sumu. Sumu inayotumika hapa ni formic acid. Sumu hii huweza kuwaua madui zao mara moja na hata kuwaumiza baadhi ya watu na kuwasababishia mzio (allergy).

G: Mateka wa Kivita.
Chungu ambao ni askari, wanapogundua kuwa wanaweza kuvamia jamii nyingine ya Chungu, na kuchukua mateka, basi hujitahidi kupigana na jamii (colony) hiyo kwa uwezo wao wote, na kumuua malkia watakayemkuta humo na kisha kuwaiba baadhi ya Chungu wenye kuhifadhi nectar na pia watayaiba mabuu (larvae), mabuu haya ni ya Chungu ambao bado hawaja totolewa. Baada ya kuyaiba mabuu haya pamoja na baadhi ya wale Chungu wenye kuhifadhi nectar, ambazo zina majimaji yenye chakula, huyafikisha kwenye makazi yao. Uko mabuu yatatunzwa na hawa Chungu (wenye nectar waliotekwa), na baada ya muda awa mabuu (larvae) watatotolewa, na baada ya kutotolewa kazi yao itakuwa ni kutafuta chakula, kutunza na kulisha Chungu wachanga walio wenyeji.
Mapigano

Je ni kwa nini basi askari wa kundi (colony) lingine hawawezi kuzuiya wizi huu wa mayai na vifukofuko (cocoons) wao? Hii inatokana na aina ya pheromone wanayotumia hawa wavamizi. (Kwani tulishaeleza hapo juu kuwa kuna aina ya pheromone, ambayo ikitumiwa huwa ni ishara ya hatari). Na pheromone inayotumiwa hapa inafanana na pheromone wanayotumia hawo Chungu wanaovamiwa. Na kinachofanyika kwa hawa wavamizi ni kuitumia kwa wingi sana hiyo pheromone ili kuwatisha hao Chungu wenyeji, ili wajue kuwa uvamizi unao fanyika ni mkubwa na wao hawawezi kumudu mapambano. Kwa hali hii itasababisha Askari wa lile kundi linalovamiwa kutaharuki na kukimbia ovyo badala ya kujilinda, na kuwaacha raia wa kawaida tu wasio na uwezo mzuri wa kujihami.

Na hii itasababisha Malkia kuuawa, mayai yake na larvae kuibiwa na wavamizi. Na kama tunavyo fahamu pheromone hutumika kwa kazi tofauti tofauti, kama vile kujua mipaka yao, kupata taarifa za sehemu mbalimbali, kujua ukubwa wa adui, na kama ishara ya kujilinda au kuvamia adui na vile vile hutumika kama alama ya tahadhari. Chungu wenye tabia hii wanaitwa “Red Amazon Ant” (Polyergus). Jamii hii ya Chungu wote ni Askari, tena ni wenye midomo mikubwa na mikali kwa ajili ya kupigana vita. Wao hawatafuti chakula wala kulea watoto wao. Kazi ya kutafuta chakula, kulea na kulisha Watoto hufanywa na mateka wa kivita. Na hata wakihama na kutafuta makazi mapya, huhama na mateka wao, kwa sababu mateka wao watatafuta makazi yalio karibu na asili yao, na hii itawasaidia hawa Red Amazon Ant kupata mateka wapya.

Red Amazon ants

Hakika katika kuumbwa mbingu na ardhi na kukhitalifiana usiku na mchana ziko Ishara kwa wenye akili, Ambao humkumbuka Mwenyezi Mungu wakiwa wima na wakikaa kitako na wakilala, na hufikiri kuumbwa mbingu na ardhi, wakisema: Mola wetu Mlezi! Hukuviumba hivi bure. Subhanaka, Umetakasika! Basi tukinge na adhabu ya Moto. 
Qur’an Surat Al I'Mran 3:190-191

Thursday, 7 June 2012

Qur'an Na Maisha Ya Nyuki


 
Na Mola wako mlezi amemfunulia Nyuki. Jitengezee majumba yako katika milima, na katika miti, na katika wanayoyajenga watu. Kisha kula katika kila matunda, na upite katika njia za Mola wako Mlezi zilizofanywa nyepesi kuzipita. Na kutoka matumbo yao kinatoka kinywaji chenye rangi mbali mbali, ndani yake kina matibabu kwa wanadamu. Akika katika haya ipo ishara kwa watu wano fikiri.
Qur’an 16:68-69

Nyuki ni wadudu ambao mara kwa mara huwa tunakutana nao katika maeneo mengi tunamoishi.Yawezekana tunakutana nao mashambani, porini, au mijini. Kwenye sura hii ya An Nah’l, katika aya ya 68-69 kuna mambo kadhaa ya kuzingatia, lakinia hapa tunayaangalia mambo machache tu, mambo ambayo watu wengi wamekuwa  hawana habari nayo na wala hawayazingatii. Japokuwa ni kwa kipindi kirefu sana, zao linalotokana na wadudu hawa, limekuwa likitumika katika chakula na mambo mbali mbali ya kimatibabu. Mfano; matibabu ya kimwili, kuongeza nguvu na nishati na kadhalika.

Basi na tuangalie kwanza neno lenyewe Annah’l, lina maana gani. Neno ili Annah’l maana yake ni Nyuki, lakini ni Nyuki wa jinsia gani? Annah’l ni jina lenye jinsia ya kike, kwa maana hiyo hicho kiumbe kilicho tajwa hapo basi bila shaka kitakuwa ni chenye jinsia ya kike. Kwa maana hiyo basi nyuki huyu tunaye muona katika harakati zake mbali mbali za kutafuta rizki ni Nyuki jike na si Nyuki dume, kama mawazo ya watu wengi wakiwemo wasomi mbalimbali wa zama hizo na zama zetu hizi. Mwaka 1600 mwandishi mmoja maarufu sana wa vitabu vya fasihi ya kiingereza (literature) aitwae William Shakespeare amemwelezea Nyuki katika kitabu chake kinachoitwa; King Henry ‘V’. Alisema hivi nanukuu, “...the King Bee goes out with his soldiers...” mwisho wa kunukuu. Yaani “...mfalme nyuki hutoka na askari zake...” neno Mfalme (King) ni neno linalotokana na watawala wa kiume, na mara nyingi utawala wa kifalme ni utawala wa kurithishana. Na kama mtawala atakuwa ni mwanamke basi hataitwa Mfalme bali ataitwa Malkia (Queen). Na pia kwa zama za kina William Shakespeare askari wote walikuwa ni wanaume, na ilikuwa si aghlabu kukuta askari wa kike. Hasa kwa miaka hiyo ya 1600 AD. Tofauti na sasa tuna askari wengi tu wa kike. Basi hebu na tuangalie wataalam wa wadudu (Entomologist) hususani, wataalam wa Nyuki wanatueleza nini kuhusu mdudu huyu Nyuki.

Wataalam wanatufahamisha kuwa Nyuki tunaowaona katika mazingira yetu ya kila siku, ni Nyuki wanawake wakiongozwa na Malkia wao ambaye pia ni Nyuki jike. Malkia ambaye ana uwezo wa kutaga mayai mpaka kufikia 3000 kwa siku, hesabu hii ni wastani wa mayai mawili kwa dakika yaani malkia wa nyuki hutaga mayai mchana na usiku. Na huyu wala si Mfalme kama mawazo ya watu wengi wanavyofikilia.

Harakati za Nyuki ni nyingi sana kwa mfano Nyuki mmoja ili atutolee kilo moja ya Asali atahitaji kufanya safari ya nenda rudi nenda rudi maili 300,000 mpaka maili 500,000. Na huwahudumia watoto wao kwa wastani wa siku sita (6). Na watoto wa Nyuki utembelewa kwa wastani wa mara 7850 kwa siku hizo sita.
 

A: Maisha ya Nyuki katika makazi yao:

maisha ya Nyuki katika mzinga wao au makazi yao na jinsi wanavyoitunza Asali isiharibike ni ya ajabu mno, maisha yao ni yenye ushirikiano mkubwa sana na wa kiwango cha juu mno. Unyevunyevu (Humidity) katika makazi ya Nyuki, ndio hukinga asali isiharibike na isipoteze ubora wake, unyevunyevu huwa katika kiwango maalum. Na kama ikitokea kuwa unyevu unakuwa mkubwa sana ama unakuwa mdogo kuliko kawaida, basi hali hii inaweza ikasababisha, asali kuharibika na kupoteza ubora wake sambamba na kupotea kwa lishe iliyomo kwenye asali. Halijoto (temperature) katika makazi ya nyuki, inatakiwa kuwa 320c. Kwa miezi takribani kumi katika mwaka. Na ili kuweza kuweka halijoto, unyevu na hewa ya kutosha katika viwango vinavyotakiwa, kuna kuwa na kundi maalum la nyuki, ambao wao wanapaswa kuhakikisha kuwa, wanadumisha hali hiyo kwa vipindi vyote vya maisha yao. Nyuki hawa moja ya kazi zao ni kuhakikisha kuwa, wanakuwa karibu na milango ya kuingilia katika makazi yao, ujikusanya na kupiga mabawa yao kwa ajili ya kingiza upepo ndani ya makazi yao, na baadhi yao huitawanya hiyo hewa ndani ya makazi na kulazimishwa upepo huo kutokea upande wa pili wa makazi yao. Kwa jinsi hiyo nyuki wanaweza kudumisha hali ya joto kwa kiwango wanachokitaka wao, na kuondoa uharibifu wa hali ya hewa (Pollution) ndani ya makazi yao.

Nyuki hawaishii kuilinda asali tu kwa kuingiza hewa na kuitoa nje kutoka ndani ya makazi yao, au kulinda na kuhakikisha kuwa unyevu na hali joto vinakuwepo katika viwango vinavyotakiwa, bali wanawajibika kuitunza asali katika kiwango kitakacholeta lishe bora kwa mlaji. Nyuki wanawajibika kuitunza asali kutokana na wadudu wa aina mbalimbali, watakao sababisha bakteria kuingia kwenye asali na kuharibu ubora wake. Siku zote wapo nyuki wanaofanya kazi hiyo ya kuhakikisha kuwa hakuna mdudu yoyote yule anaeingia katiaka nyumba yao, na kuiharibu asali yao. Na kama ikitokea kuwa kuna mdudu au kitu chochote kile, kimeingia kwenye asali, basi nyuki watashirikiana kukishambulia kitu hicho ili kitoke, na kama kitu chenyewe ni kidogo basi watakitoa nje. Kama ikitokea kuwa kitu hicho au mdudu huyo ni mkubwa kiasi ya kwamba wao kwa uwezo wao wanashindwa kukitoa au kumtoa nje ya makazi yao, basi watatumia njia nyingine ya kuilinda asali yao na makazi yao kwa ujumla. Njia watakayo tumia nyuki hao ni kutengeneza ute (Bee Resin) na kuuchanganya na utomvu unaotokana na miti au baadhi ya mimea kama vile, miti ya misonobari (Pine tree), mpopla (Poplar tree) au mti unaoitwa Acacia tree. Kutokana na miti hiyo hutengeneza kitu kinachoitwa Propolis. Propolis ni dawa ambayo ina uwezo wa kuzuia bakteria wa aina yoyote ile asiharibu asali. Watakacho fanya sasa baada ya kutengeneza Propolis ni kukizungushia au kumzungushia mdudu huyo ute huo ambao huwa kama gundi ngumu yenye rangi nyekundu, bila ya kubakisha upenyo hata mmoja, yaani watamzungushia mwili mzima, kwa unene wa milimita moja na nusu 1.5mm. ili kuikinga asali na uharibifu utakaotokea au kusababishwa na kitu hicho au mdudu huyo. Vilevile kama kutatokea nyufa katika mzinga wao, basi hutumia ute huo huo kuzibia nyufa hizo, ute huo unapokutana na hewa ya nje, huganda mara moja na kuwa mgumu sana ili kuzuia baadhi ya wadudu wadogo wadogo na bakteria wa aina mbalimbali wasiweze kuingia ndani ya mzinga, na kuharibu asali.

Haya ni mambo makubwa kabisa kufanywa na wadudu wadogo kama hawa. Ama kwa akika Mwenyezi Mungu ni mkubwa na mwenye Rehma nyingi. Kwa kuwapa iliham wadudu hawa ili waweze kuifanya kazi hii bila ya kuchoka wala kutegeana. Kama anavyosema Mwenyezi Mungu kuwa amewafunulia nyuki, kuwa wajitengenezee majumba yao katika milima, katika miti na katika wanayoyajenga watu na ale kila matunda ili haweze kutengeneza chakula kilicho bora na kilicho na dawa (matibabu/ponyo) ndani yake. Alhamdullilah kwa akika hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kila hali.

B: Mzinga wa Nyuki:

Nyuki katika mzinga mmoja hufikia idadi ya nyuki wanaokisiwa kuwa 30,000 na zaidi. Nyuki wanapokuwa katika moja ya kazi zao za kutengeneza masega, huyaweka katika mwinuko wa nyuzi 130, kwapande zote mbili. Na nyuki huepuka kuweka masega sambamba na ardhi ili asali isimwagike chini. Nyuki hujining’iniza na kujishikiza wenyewe kwa wenyewe na kuwa kama duara kuzunguka mzinga wao, katika kila kona ya mzinga. Kwa kufanya hivi husababisha halijoto ya ndani ya mzinga kufanya hutengenezaji wa masega na nta kuwa rahisi. Nyuki uchota nta kwa kutumia miguu yao, iliyo na kama ndoana mbele na kuchanganya na majimaji yanayotoka matumboni mwao. huichanganya nta na majimaji hayo kwa kutumia midomo yao, mpaka kuwa laini ili waweze kuipaka katika kuta za masega yao ya asali. Masega hutengenzwa kuanzia pande nne tofauti tofauti juu kuja chini, toka pande tofauti katika mzinga na kuishia katikati. Na kupata usawa katika masega bila kukosea. Jambo ili la kutengeneza masega na mtindo wanaotumia wa kutengeneza masega yenye umbo la pembe sita limewashangaza wataalam mbalimbali wa kisasa. . Tena hutengeneza bila ya kukosea vipimo. Hutengenezaji ambao kwanza huanza katika kona tofauti tofauti pia kwa vikundi vikundi na kuelekea katikati. Je watu wa elimu ya Nadharia ya evolusheni (Evolution theory) wanayajua haya?  Soma Qur’an 45:4

 Na katika umbo lenu na katika wanyama alio watawanya zimo ishara kwa watu wenye yakini…
Qur’an 45:4

Umbo ili la heksagoni linafanana na kichwa cha nati ya gali (bolt) na kama tulivyo eleza hapo juu kuwa, kila tundu moja la linanfanana na mwenzake. Japokuwa matundu yapo kwa maelfu. Uhandisi huu wa ajabu ambao unaonyeshwa na viumbe hivi vidogo wafaa kuzingatiwa sana na binadamu, juu ya kuwepo Mwenyezi Mungu. Matundu au masega kama yanavyo julikana, kazi yake kubwa ni kuwatunzia watoto wa nyuki, na kuifadhia asali. Katika mamilioni ya miaka nyuki wamekuwa ni watengenezaji wazuri wa asali, wasio wezwa kuigwa. Yaani ni bidhaa hiliyo bora kabisa isiyo na mpinzani wala mwigizaji aliyejaribu kutengeneza kitu kinacho fanana nacho. Hutengenezaji huu wa asali ya nyuki ni wa miaka zaidi ya milioni nyingi tu lakini sasa kwa nini wame chagua kutengeneza masega yenye umbo la pembe sita zilizo sawa yaani hexagon na si umbo lingine lolote lile mfano wa pembe tatu (Triangle) au pembe nane (Octagon) au pembe tano (Pentagon)? Jibu lake wanalo watu wa mahesabu ya maumbo (mathematician), wao wanasema hivi...

Umbo la hexagon yaani umbo lenye pembe sita zilizo sawa, ni umbo bora na ni zuri sana katika mahesabu ya jiometri. Kwa sababu huchukua nafasi ndogo, lakini huwa na ujazo mwingi katika eneo lake. Na ufanisi wake katika matumizi ni mzuri kwani umbo ili haliachi nafasi isiyoweza kutumika, tofauti na maumbo mengine. Kina chake kiko sawa kwa masega yote ya nyuki, na vilevile mzingo wake yaani mzunguko wake ni mdogo na mfupi na ujazo wake uko sawa. Vilevile hutumia nta kidogo katika kutengeneza masega yao, ukilinganisha na maumbo mengine kama pembe tatu au pembe nne. Kwa hiyo tunaona kuwa umbo la heksagoni hutumia nta kidogo sana wakati wa kutengeneza masega lakini wakati huo huo uhifadhi asali nyingi.  Jibu ili wataalamu wa hisabati katika eneo linalohusiana na hisabu za jiometri wamelipata baada ya tafiti nyingi na za miaka mingi sana. Lakini kwa uhakika ulio wazi kabisa hesabu hizi za kutengeneza masega katika umbo la pembe sita sawa (hexagon), hawakufanya nyuki wenyewe binafsi yaani kwa utashi wao tu, bali ni kutokana na maumbile yao aliyo waumbia Mwenyezi Mungu, kwa sababu tunaelezwa kwenye Qur’an 16:68 kuwa:

Na Mola wako mlezi amemfunulia Nyuki: Jitengenezee majumba yako katika milima, na katika miti, na katika wanayo jenga watu... Qur’an 16:68

Isitoshe basi umbo la hexagon katika masega ya nyuki jinsi lilivyo matundu yake yanategemeana yaani umbo kwa umbo kuta kwa kuta na kuta zake ni nyembamba na zinahimili ujazo mkubwa wa asali.


Picha ya masega ya Nyuki nyuzi digrii 130

C: Jinsi nyuki wanavyo wasiliana:

Mawasiliano waliyokuwa nayo wadudu hawa, ni ya kiufanisi wa hali ya juu sana. Kwani utaratibu wao wa kuwasiliana ni wa ajabu mno. Nyuki siku zote husafiri umbali mrefu, ili kujitafutia eneo la malisho (mavuno) yao yaani Necta na Chavua. Nectar ni majimaji yanayopatikana kwenye maua, pamoja na Chavua (flower dust or pollen). Nyuki wana uwezo wa kwenda zaidi ya kilomita mbili, toka katika mzinga wao na kurudi. Nyuki aliyeko mawindoni anapogundua eneo la mavuno (maua), huruka kurudi mzingani ili kuwafahamisha wenzake, ni wapi na ni umbali gani toka kwenye mzinga mpaka kwenye mavuno yao. Je ni jinsi gani basi nyuki huweza kutaarifiana, umbali na eneo yalipo mavuno yao? Wataalam wa nyuki baada ya kuwachunguza wadudu hawa kwa kipindi kirefu, wamegundua kuwa nyuki utaarifiana kwa kutumia vitendo na harufu. Mawasiliano haya ya vitendo yapo ya aina mbili, nayo huitwa (Waggle & Round Dance), yaani mawasiliano ya kujitikisa na kujizungusha kwa kuchachawa.

Angalia mchoro hapa chini.
(Picha ya nyuki wakiwasiliana kwa namna mbili tofauti)

Mchoro wa kushoto chini unaonyesha mawasiliano ya kujizungusha kwa maana ya duara (Round Dance). Kabla ya yote yale, nyuki hukimbia huku akielekea kule kwenye mawindo (First it runs straight for short distance, the angle of the run indicating the direction of the source). Na hapo uchezesha tumbo lake pamoja na kuchezesha eneo la nyuma, kabla ya kufanya mzunguko wa kutengeneza duara. Na hii inamaanisha kuwa mawindo yao hayapo mbali ni chini ya mita mia (100). Na mchoro wa pili kulia juu ni mawasiliano ya kujitikisa na kuzunguka (Waggle Dance), na kuwa kama wanatengeneza umbo la namba nane, kuna maanisha kuwa mawindo yao yapo mbali, yaani zaidi ya mita mia moja (100). Kwa hiyo mapigo ya kuchezeza miili upokezana wao kwa wao, mpaka wote wanakuwa wameelewa ni wapi na kwa umbali gani, na pembe (angle) gani mawindo yao yanapatikana. Mfano wakitaka kufahamishana umbali wa mita 250, basi huchezesha eneo la chini ya tumbo mara tano kwa nusu dakika. Unaweza ukajiuliza kuwa, je hawa nyuki mbona hata usiku huwa wakiruka na kufanya harakati zao? Jibu lake ni rahisi tu. Ni kuwa macho ya nyuki jinsi yalivyo umbwa kwanza yana umbo la pembe sita (hexagon) na yapo zaidi ya mia, yenye lenzi zinazo jirekebisha zenyewe (involuntarily), kila baada ya dakika moja, ili kuwa sambamba na machweo ya jua. Kwa jinsi hii ya maumbile ya macho yao, nyuki hawawezi kupoteza mwelekeo wao hata mara moja, hata wakiruka hewani kwa zaidi ya dakika  kumi na tano (15). Vilevile macho ya nyuki yanasaidiwa na mionzi inayoitwa utraviolet rays. Kutokana na na mionzi hii inakuwa ni rahisi kwao kufanya kazi hata kwenye kiza.

               Aina ya pili ya mawasilano ya nyuki kama nilivyo ainisha hapo juu, ni kwa kutumia harufu, nyuki wanauwezo mkubwa wa kuhisi (sentient). Nyuki huwa hawana muda wa kupoteza katika kazi zao. Kwani nyuki hata siku moja huwa hawatui kwenye ua ambalo limekwisha tembelewa na nyuki mwenzake, kwa maana ya kuwa limekwisha tolewa chamvua. Ni vipi basi nyuki ufahamu kuwa ua analotaka kutua limekwisha tembelewa na mwenzake, na kuamua kulipita bila ya kupoteza muda kwenye ua hilo? Ili ni jambo dogo sana kwao, kwani nyuki anapotua kwenye ua na kuchukua alichofuata hapo, uacha harufu (Pheromones) kwenye ua hilo ili kila nyuki apitae hapo atambue na kufahamu kuwa ua analolipitia limekwisha tembelewa tayari. Kwa hali hiyo anakuwa hana muda wa kupoteza nguvu zake hapo.   

D: Ubora wa asali:

Makisio ya hutengenezaji wa asali kwa mwaka kutokana na idadi ya nyuki milioni hamsini (50 million), ni tani zipatazo 900,000 (haya ni makisio ya mwaka 2000 kutoka kitabu cha Leader’s Digest kiitwacho Why in The World?). Wataalamu kwa karne nyingi wamejaribu kutengeneza asali, lakini wameshidwa na hii ni kutokanan na asali kuwa na michanganyiko mingi ya sukari na virutubisho vya kiasili. (The bees’ way of making honey, too, is complex and difficult to copy). Hebu basi na tuangalie tunapata nini kutokana na asali, kwani Mwenyezi Mungu ametatufahamisha kwenye Qur’an 16:69 kuwa

…Na kutoka matumbo yao kinatoka kinywaji chenye rangi mbali mbali; ndani yake kina MATIBABU kwa wanaadamu. Akika katika haya ipo ishara kwa watu wanao fikiri.
Qur’an 16:69

 Asali ni chakula bora cha kiwango cha juu sana ambacho, Allah (swt) ametuteremshia kupitia wadudu hawa aina ya nyuki. Na vilevile tunafahamishwa katika sura hii ya 16 kuwa asali ina uwezo wa kutibu. Sasa basi Asali ni nini? Asali ni mchanganyiko wa virutubisho mbali mbali, zikiwemo aina ya sukari zinazojulikana kwa jina la Glukosi (Glucose) pamoja na Fruktosi (Fructose), na madini mbalimbali vikiwemo; Magnesium, Copper, Iodine, zinc, Potassium, Calcium, Sodium, Chlorine, Sulfur, Iron na Phosphate, pamoja na vitamin B1, B2, B3, B5, B6, na vitamin C. Vitamin mara nyingi ubadilika kulingana na ubora wa necta, pamoja na chavua. Vile vile kwenye asali, kunapatikana aina mbalimbali za Hormones. Kama inavyoelezwa kwenye Qur’an, kuwa asali ni ponyo(kinywaji chenye kutibu) kwa wanadamu, na haya yamethibiti kwa wanadamu hivi leo. Kama ilivyotokea katika mkutano wa wanasayansi,  uliofanyika mwaka 1993 mwezi Sept. tarehe 20-26. Mkutano huu ulifanyika nchini China, na ulijulikana kwa jina la World Apiculture Comference. Na kuchapishwa katika jarida la Horriget News Paper, la tarehe 19th.Oct.1993. Katika mkutano huo matibabu ya kutumia asali yalijadiliwa kwa mapana sana, wanasayansi wa Kimarekani wao walielezea kuwa, ndani ya asali kuna vitu vinaitwa; Royal Jelly, chavua, na ute (Propolis, Bee resin), vitu hivi husaidia sana katika matibabu ya magonjwa mengi. Naye Daktari kutoka Romania, yeye aliwahi kujaribu kutibu mtoto wa jicho (Cataract), kwa wagonjwa 2094, kati yao 2002 walipona kabisa, na hii ni sawa na asilimia 96% ya wagonjwa waliopona kabisa. Daktari huyo alieleza kuwa Bee Resin au ute unaotokana na nyuki, unasaidia kuponyesha magonjwa mengine, mfano magonjwa ya ngozi (Skin Diseases), magonjwa ya kuvuja kwa damu (Haemorrhoid), magonjwa ya uzazi (Gynaecological Diseases) n.k.

 Siku hizi ufugaji wa nyuki kwa ajili ya kufanya tafiti mbalimbali za kisayansi umeongezeka kwa kiwango cha juu sana, katika nchi zilizo endelea na zinazo endelea. 


E: Baadhi ya faida nyingine za asali:

  • Sukari iliyoko kwenye asali humengenyuka kwa urahisi sana, na kugeuka kuwa glukosi na fruktosi kwa haraka. Hata kwa wale wenye matumbo mabovu (yenye maradhi).
  • Asali husaidia pia figo na utumbo kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.
  • Asali ina kalories chache sana, ukilinganisha na kiwango cha sukari kilichomo kwenye asali, cha ajabu ni kuwa hutoa nishati (energy) nyingi katika mwili, lakini haisababishi ongezeko la mwili yaani unene. (Cholesterol)
  • Asali huyeyuka kwa haraka sana kuingia kwenye damu, ukilinganisha na vinywaji vingine, kama maji ya kawaida.  Asali huchukua takriban dakika saba tu kuingia katika mfumo wa damu.
  • Asali husaidia hutengenezaji wa damu mwilini, kwani hutoa nishati au nguvu inayosababisha hutengenezaji wa damu kuwa rahisi. Vilevile asali usafisha damu, katika mzunguko wake, na kusaidia mzunguko wa damu kuwa rahisi na mwepesi. Asali husadia kulinda mishipa ya damu isiathirike na maradhi yanayoshambulia mishipa ya damu. Asali pia husaidia kulinda ubongo na kuuwezesha kufanya kazi vizuri na upesi zaidi. Asali husaidia kuua bakteria wa aina mbalimbali inapotumiwa kwa matibabu na hasa kwenye vidonda. Pia asali husaidia kuondoa matatizo ya tishu (Tisue Difficiency) na udhaifu kwenye mwili (Body Frailty).

Qur'an 5:32