Wednesday 2 September 2015

Muujiza wa Kisayansi Surat Kahf


Nawe utawadhania wamacho, na hali wamelala. Nasi tunawageuza kulia na kushoto. Na mbwa wao amenyoosha miguu yake ya mbele kizingitini. Kama ungeli watokea hapana shaka ungeli geuka kuwakimbia, nawe umejaa khofu. 
Qur'an, 18:18

Ayah hii hapo juu inahusu kisa cha watu wa pangoni, waliolala usingizini kwa mamia ya miaka. MwenyeziMungu anatufahamisha kuwa alikuwa akiigeuza geuza miili yao kushoto na kulia. 

Kuna Hikma gani mtu au mgonjwa anapolala na kugeuzwa geuzwa au kugeuka geuka upande huu na ule kila baada ya muda Fulani? Je kibaiolojia kuna faida gani kiafya, unapolala na kujigeuza geuza na kuna hasara gani ukilala muda mrefu bila ya kujigeuza geuza?

Ikitokea mtu akalala kwa kipindi cha muda mrefu bila kujigeuza/kugeuzwa kama mtu aliyeko kwenye coma (unconsciousness) kwa kupoteza fahamu, upatikana na matatizo makubwa ya kiafya, kama vile matatizo ya mzunguko wa damu, vidonda mwilini, na kuganda kwa damu (Blood clotting) katika sehemu ile iliyochini, kwa maana upande ule aliolalia.1*

Vidonda hivi kitaalam ujulikana kama "bed sores au pressure sores." Vidonda hivi ujitokeza au usababishwa na mgandamizo wa muda mrefu, pale mgonjwa au mtu aliyelala na kupoteza fahamu (Coma) bila ya kujigeuza au kugeuzwa geuzwa mara kwa mara. Hali hii upelekea mishipa ya damu kujisonga au kugandamizwa kwa kipindi kirefu, mishipa ya damu inapo banwa kwa muda mrefu mzunguko wa damu uwa mdogo sana, na wakati mwingine usababisha mishipa ya damu kuharibika kabisa. Matokeo yake, oksijeni na virutubisho vingine ambavyo utegemea mzunguko wa damu ili kurutubisha mwili kushindwa kuifikia ngozi, na baada muda ngozi huanza kukosa uhai na hatimaye kufa/kuharibika.

Hali hii ndio inapelekea kupata vidonda mwilini chini ya ngozi (bed sores au pressure sores), dalili za mwanzo ni maumivu kwenye ngozi na hata misuri na mafuta (Body Fat) mwilini uweza kuhathirika.2*


Kama hali hiyo haikutibiwa mapema vidonda hivi,uendelea kwenye tishu za nyama na hata kufikia kwenye mifupa. Vidonda hivi vikiachwa bila kutibiwa vinaweza kuleta matatizo makubwa kwenye mwili wa muhusika na hata kusababisha kifo.

Kinachotakiwa kufanywa ili kuepusha matatizo yote hayo ni kwa mgonjwa kujigeuza geuza kila baada ya muda mfupi (dakika 15) ili kupunguza shinikizo la mwili. Na kwa wagonjwa ambao hawawezi kujigeuza wenyewe wanapaswa wasaidiwe kugeuzwa kila baada ya masaa kadhaa.3*

Wanasayansi wameyagundua haya, miaka hii ya karibuni tu, wakati Qur’an imeonyesha umuhimu wa mtu anapolala na kujigeuza au kugeuzwa ili asipatikane na matatizo ya kiafya, haya yameandikwa zaidi ya karne 14 zilizopita.

Reference:

  1. http://www.webmd.com/skin-problems-and-treatments/four-stages-of-pressure-sores
  2. http://jama.jamanetwork.com/article.aspx?articleid=195719
  3. Kenneth Davis, Jr., et al. “The Acute Effects of Body Position Strategies and Respiratory Therapy in Paralyzed Patients with Acute Lung Injury,” Critical Care 5 (2001): 81-87, http://www.ccforum.com/content/5/2/81.

No comments:

Post a Comment

Qur'an 5:32