Tuesday 27 September 2016

BINADAMU NA UPATIKANAJI WA MVI KATIKA QUR'AN


Msongo wa mawazo katika maisha yetu ya kila siku.

Sayansi Inathibitisha Kutoka Mvi kwa Haraka kama Ilivyoelezwa Ndani ya Qur’an

'MSONGO WA MAWAZO na HUZUNI,' ndio ugonjwa wa zama hizi, si maradhi yanayoishia kisaikolojia tu. Bali madhara yake hujidhihirisha katika kiwiliwili kwa njia mbalimbali. Matatizo makubwa yanayohusishwa na dhiki na huzuni ni magonjwa ya akili, madawa ya kulevya na utegemezi, kukosa usingizi, maradhi ya ngozi, maradhi ya tumbo na shinikizo la damu, kipandauso, magonjwa ya mifupa, matatizo ya figo, pumu, kudhuru, maradhi ya moyo na matatizo katika ubongo.

Na inawezekana kabisa maradhi haya yasitokane na 'Msongo (Stress) na huzuni'. Hata hivyo, imethibitika kisayansi kuwa Msongo na huzuni,' mara nyingi ndio chanzo cha maradhi haya.

Msongo ni hisia zote kwa ujumla zinazosababishwa na hofu, kukosa amani, kukata tamaa, msisimko mkubwa, wasiwasi na shinikizo pale uwiano unapokusekana mwilini. Watu wanapopata Msongo, miili yao inapigana na kutoa ishara. Msongo isiyokwisha inaweza kusababisha uharibifu mkubwa mwilini na kuusababishia kutofanya kazi zake ipasavyo. Mfano wa athari zinazopatikana wakati mwili haufanyi kazi sawasawa ni kutoka mvi haraka. Allah anathibitisha haya ndani ya Qur'an:

Basi nyinyi mkikufuru, mtawezaje kujikinga na Siku ambayo itawafanya watoto wadogo waote mvi?
(Surat Al-Muzammil [73] 17).

Katika aya hii, Allah anatuonyesha athari ya msongo katika nywele zetu kwa kuainisha madhara ya hofu ya siku ya kiama, ambapo itawafanya hata watoto nywele zao ziote mvi. Ukweli huu aliotuelezea  Allah kisayansi tayari umethibitishwa na siku na zama tulizonazo. Hebu tuone namna nywele zetu zinavyobadilika na kufanya mvi.

VIPI NYWELE ZINAFANYA MVI?

Kuna aina mbili za melanin ambazo huzipa rangi nywele zetu. Moja ni 'eumelanin,' ambayo huzipa rangi nyeusi, na nyingine ni 'pheomelanin,' ambayo huzipa nywele rangi nyeupe. Kadri umri unavyoongezeka, seli katika ngozi ya kichwa zinapungukiwa uwezo wa kutengeneza melanin na hivyo nywele zinapoteza rangi yake na kugeuka kijivu. Wakat baadhi ya nywele zimebakia na rangi yake nyeusi, nyengine zinageuka rangi nyeupe hasa kwa watu wenye nywele nyeusi,  nywele zao zinaonekana zikiwa katika rangi mbalimbali za kijivujivu.

Ingawa sayansi haijabainisha kwa ukamilifu mifumo ambao nywele zinapitia hata kuwa nyeupe, imeonekana kuwa matumizi ya Hydrogen peroxide katika saluni huzifanya nywele ziwe nyeupe. Seli zinazozalisha melanin pia huzalisha hydrogen peroxide ambayo kikawaida huvunjwavunjwa na enzyme inayoitwa catalase. Kadri umri unapoongezeka, kiwango cha catalase kinapungua na mkusanyiko wa hydrogen peroxide unazuia utengenezwaji wa melanin. Matokeo yake huwa ni nywele kubadilika na kuwa nyeupe. Basi ni jinsi gani utaratibu wa kisaikolojia unafanyakazi kwa haraka na kuzibadilisha nywele rangi yake?

MSONGO WA MAWAZO IMETHIBITISHWA KISAYANSI KUZIFANYA NYWELE ZIWE NA MVI

Kichwa wakati mwingine huingia mvi kutokana na hofu au mshtuko au wakati mwingine huwa ni matokeo ya dhiki zisizokwisha. Hii hali ya kubadilika ghafla kwa nywele, inajulikana kama 'canities subita' inahusu zaidi nywele kupoteza rangi hali ile nywele ilopoteza rangi inabakia palepale. Hivi ndivyo  jinsi gani inavyotokea.

Ugonjwa unaojulikana kama 'alopecia areata' ni matokeo ya kunyonyoka nywele na kufanya kipara. Harakati za mfumo wa kinga ya mwili kupambana wenyewe kwa wenyewe husababisha maradhi haya. Msongo wa mawazo ndio  sababu inayochochea hali hii.

Wanasayansi wanaifanyia uchunguzi hoja kuhusu sababu ya mfumo wa kinga mwilini inayohusishwa na uzalishwaji wa rangi katika nywele. Nywele nyeupe zilizoshwindwa kuzalisha rangi haziathiriki na mfumo wa kinga mwilini, wakati nywele nyeusi ndizo zinazoathirika na ugonjwa huo. Nywele nyeupe hubaki, na kwa kawaida katika hali hii nywele hubadilika ndani ya mwaka mmoja au miezi tu.

Nywele za watu ambao wanapata ghafla matatizo ya hofu na mshtuko wakati mwingine zinageuka kuwa  nyeupe kwa siku moja au siku chache tu. Sababu ya nywele kugeuka nyeupe kwa njia hii imetolewa ufafanuzi na kikundi cha watafiti kikiongozwa na mshindi wa tuzo ya Nobel kwenye kemia Robert Lefkowitz. Utafiti juu ya panya ulionyesha kuwa matatizo yasokwisha yanaharibu mfumo wa DNA, na jambo hili hupelekea nywele kugeuka nyeupe. Kadri dhiki na msongo wa mawazo inavyokuwa kubwa zaidi, ndivyo uharibifu mkubwa unapatikana katika DNA, na nywele zinabadilika kuwa nyeupe kwa kasi.

Allah  anatufahamisha kuwa Dhiki (Msongo wa Mawazo, yaani STRESS) inayosababisha matatizo mbalimbali ya mwili na akili ikiwa ni pamoja na nywele kutoka mvi huwapata watu walioipa mgongo DINI (UISLAM) kama tunavyo fahamishwa ndani ya ayah hii...

"Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu."
(Qur'an Surat T'aha [20] 124). 

Allah anatufahamisha kuwa wale watakao kufuru atawafanyia vikwazo katika mambo yao na kuwafanyia maisha magumu. Katika ayah nyingine Allah anatuambia;

"...Na pia wale watatu walio achwa nyuma hata dunia wakaiona dhiki juu ya ukunjufu wake, na nafsi zao zikabanika, na wakayakinika kuwa hapana pa kumkimbia MwenyeziMungu isipo kuwa kwake Yeye. Kisha akawaelekea kwa rehema yake ili nao waendelee kutubu. Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kupokea toba na Mwenye kurehemu.
(Qur'an Suratut Tawba [9] 118)

Haya maisha ya tabu au maisha ya dhiki kama tuyaitavyo leo, ni matokeo kwa wale wasioamini, wanaoishi maisha yalio nje ya maadili ya imani. Leo madaktari wanatuambia kwamba amani na utulivu wa akili ni muhimu kwa ajili ya kuepushwa na madhara yatokanayo na Msongo wa mawazo, raha na utulivu wa akili vitapatikana tu pale mtu atakapoifanya Qur'an kuwa ni sehemu ya maisha yake ya kila siku na kumkabidhi kila kitu Allah.

Allah anatuonyesha haya katika aya mbalimbali ndani ya Qur'an kuwa atawapa amani na utulivu Walioamini.

"...mna ndani yake kituliza nyoyo zenu, kitokacho kwa Mola wenu Mlezi..."
(Surat al-Baqarah [2] 248

"...Kisha Mwenyezi Mungu akateremsha utulivu wake juu ya Mtume wake na juu ya Waumini..."
Suratut Tawba [9] 26

"...Usihuzunike. Hakika Mwenyezi Mungu yu pamoja nasi. Mwenyezi Mungu akamteremshia utulivu wake..."
Suratut Tawba [9] 40

"Yeye ndiye aliye teremsha utulivu katika nyoyo za Waumini ili wazidi Imani juu ya Imani yao..."
Surah Fath[48] 4

"... Basi akateremsha utulivu juu yao, na akawalipa kwa Ushindi wa karibu."
Surah Fath[48] 18

ALLAH AMEAHIDI KWA WAUMINI KAMA IFUATAVYO:
"Mwenye kutenda mema, mwanamume au mwanamke, naye akawa ni Muumini, tutamhuisha maisha mema; na tutawapa ujira wao kwa bora ya waliyo kuwa wakiyatenda..." 
(Surat-Nahl [16] 97)

No comments:

Post a Comment

Qur'an 5:32