Tuesday 6 March 2012

Zama za Mawe


Kwa mujibu wa wanahistoria wa mambo ya kale, wanatufahamisha kwamba zana za Mawe kilikuwa kipindi kirefu cha historia ya kale ya ubinadamu. Watu hawakutumia vyuma (metali) bado hivyo walitumia mawe pamoja na mbao na ngozi kwa kutengeneza vifaa mbali mbali. Kuna mabaki mengi ya mawe yaliyochongwa kwa matumizi kama vifaa na mabaki hayo yamekuwa msingi wa jina "zama za mawe".

Kwa hiyo ni kipindi cha matumizi ya mawe yaliyochongwa kuwa vifaa baada ya kipindi ambako watu walitumia fimbo tu au mawe katika hali asilia na kabla ya kipindi watu walipoelewa kutumia zana zilizotengenezwa kwa chuma (metali).

Zama za mawe zilikuwa vipindi virefu sana cha miaka mia elfu nyingi. Wataalamu wamegawanya zama hizi katika vipindi mbalimbali kama Zama za mawe za kale na Zama za mawe za kati lakini wataalamu wa siku hizi wanaona ya kwamba mgawanyo huu ulitazama zaidi historia ya Ulaya isiyolingana na historia ya sehemu nyingine za dunia.

Tatizo kuu la mafundisho haya ni kwamba yameangalia upande mmoja wa dunia na kusahau kuwa dunia illikuwa na watu karibia pande nyingina maendeleo ya teknolojia yalitofautiana sana, kama ilivyo hivi leo. Kuna mataifa yameenendelea sana na mengine yapo nyuma, kiasi mtu akipiga picha anaweza kufikiria kuwa hizo ni picha za miaka zaidi ya milioni iliyopita.

Ili ni kosa kubwa walilolifanya wataalam wetu wa historia ya mambo ya kale. Kwa kukosa kwao kuangalia pande nyingine za maendeleo ya kibinadamu, kumepelekea kutuletea tafiti ambazo zinajikanyaga..

Kwa mfano chuma haikutumiwa huko Amerika hadi karne ya 16 na huko Pasifiki hadi karne ya 17. Hata hivyo jamii za Amerika kama Azteki au Wainka walikuwa na teknolijia nyingine mbalimbali waliweza kudumisha miji mikubwa kushinda miji ya Ulaya ya wakati ule.

Hata hivyo neno "zama za mawe" limekuwa ni neno la kawaida duniani, na wataalamu wanaendelea kulitumia wakijua kasoro zake kwa sababu hadi hasa hakuna neon linguine lenye kufaa zaidi ya ili.

Tuangalie basi kipindi hicho walichokiita zama za mawe yaani Stone Age. Kwa hakika kabisa ukiangalia tafiti za wakati huu utagunduwa kuwa duniani hakujawahi kutokea zama walizo ziita zama za  mawe, kwa sababu kila magunduzi mapya yanayofanyika tunaona kuwa watu hawa walioitwa wa zama za mawe walikuwa wakiishi maisha yaliyo kamili kabisa bila ya wasi wasi wowote ule mfano walikuwa wakiishi kifamilia kama ivi leo tunavyoishi na pia walikuwa wakipika vyakula vyao kwa kutumia majiko ya moto, wakitembelea majirani zao, wakitibiwa na madaktari wao, wakiimba na kucheza muziki, wakishona nguo, kujishughulisha na kazi za sanaa mbali mbali kama kufinyanga, kuchonga, na ufuaji wa vyuma.


Miko na shanga ilotumika miaka 12,000BC ilopita.

Ebu angalia hapa kushoto picha ya mkufu uliotengenezwa kwa mawe na masimbi ya baharini. Je haitoshi kujiuliza ndani ya nafsi zetu ni vipi watu hawa waliweza kutengeneza mkufu kama huu? 

 Ebu angalia mwiko, picha iliyo hapa chini kushoto, vifaa ivi vina miaka 7-11,000 BC Je haitoshi tu kuamini kuwa binadamu hawa walikuwa kama sisi tu na hakuna tofauti yoyote ya msingi? Kulingana na wana evolusheni kipindi hiki binadamu halikuwa hana uwezo bado wa kutengeneza zana kama hizi. Lakini kila kukicha wataalamu wa (archaeology) akiolojia yaani elimu ya mambo ya kale wanagunduwa mambo mapya kuhusu binadamu hao tunawaita wa kale. Na kutuonyesha kuwa binadamu hao walikuwa wameendelea katika nyanja mbali mbali kwani inaonyesha kuwa walikuwa wakitumia meza, vijiko uma, vikombe, sahani na mabakuli kama tunavyo tumia ivi leo. Wataalamu wa akiolojia wamegunduwa mawe haya (angalia picha hapo chini) ambayo yalikuwa yakitumika kama shanga amabayo yana miaka 12,000 BC ebu tizama matundu ya shanga na vifungo 


vilivyotobolewa kiustadi, je uwezi kujiuliza waliwezaje kutoboa tundu za shanga na vifungo hivi kama watu hawa walikuwa hawana tekinolojia yoyote ile zaidi ya kutumia mawe kugonga gonga tu? Kwa hakika watu hawa walikuwa na zana madhubuti za chuma zilizo wawezesha kutoboa matundu kama haya.



Picha za filimbi kushoto zina umri wa miaka 95,000 na hii inatujulisha kuwa watu hawa walikuwa wanatumia ala za muziki kama firimbi na kadhalika.



Angalia msharasi huu kigingi (Awl, picha ya juu) kilicho tengenezwa kwa shaba halisi watu hawa walikuwa na utaalamu wa kutosha kujuwa kuwa shaba haipati kutu ndo mana wakatumia kama sindano za kushonea na hii pia inatujulisha watu hawa walikuwa na uwezo wa kuchimba madini mbali mbali kwa matumizi yao ya kila siku.

Miaka zaidi ya laki moja na zaidi binadamu alikuwa akiishi ndani ya majumba wakijishughulisha na kilimo wakibadilishana bidhaa mbali mbali kama vile nguo bidhaa za mashambani na kadha wa kadha. Inaonyesha kuwa baadhi yao walikuwa wanaafanya ibada kama ivi leo na wengine walikuwa si watu wa ibada. Na hii inaonyesha hata ivi leo kuna walio endelea kisayansi na wapo wanaoishi nyuma na maendeleo na hii ipo tangia dunia ilipoumbwa na kuwepo binadamu. Na ebu tizama ulimwengu huu wa leo tunao huita wa sayansi na tekinolojia, kuna baadhi ya nchi zinarusha vyombo angani kwenda kwenye sayari na kuna nchi hata umeme mashaka kwao, nah ii haina maana kuwa watu waliokuwa katika nchi zisizo endelea au zinazoendelea kuwa akili zao ni duni na wale walio katika nchi zilizo endelea akili zao ni nzuri sana la hasha haya yote ni mipango yake Mwenyezi Mungu ili binadamu tupate kutegemeana na tuweze kumtambua muumba wetu.



Juu kushoto na kulia ni picha zilizopigwa mwaka 1895, jijini NewYork.

Kushoto ni picha ya Aborigines kutoka Australia) ni picha iliyopigwa mwaka 1895.

Chini ni Wahindi kutoka kanda ya mashariki mwa Sepahua Peru, Mwaka 1984




Hapa juu kuna vitu vilivyotengenezwa kwa maru maru na barsalt na bangiri amabazo zinakisiwa kuwa na umri wa miaka 8500-9000 BC. Kwa mujibu wa wana evolusheni kipindi hiki binadamu alikuwa hana uwezo wa kutengeneza zana kama izi na kwa kuzingatia kuwa barsalt ni madini ngumu sana kuitengenezea umbo lolote kwa kutumia mawe tu. Na hapa tumeona mkufu, bangiri na vifaa vingine ambavyo vinaitaji vifaa vilivyo vigumu na utaalamu kuvitengeneza.

  1. Mawe ya nakshi (Stone mosaic fragments) yanakisiwa kuwa na umri wa miaka 10,000 BC
  2. Kinu na mchi wenye umri wa miaka 11,000 BC
  3. kifaa kilicho tengenezwa kwa madini ya kioo (An obsidian tool). Kifaa hiki kina umri wa miaka 10,000BC. Je ni rahisi kweli watu hawa tunaowaitwa wa zana za mawe waliweza kutengeneza kifaa kama hiki kwa kuponda ponda tu bila ya kuwa na dhana nzuri kwa kazi hii?
  4. Vifaa vilivyhotengenezwa kwa miamba 11,000 BC
  5. Simbi lilotobolewa lilokana na malakati 9-10,000 BC
  6. Sifongo yenye umbo kama msumali ilotengezwa kutokana na jiwe 10,000 BC
  7. Kichwa cha nyundo umri 10,000 BC.

 Angalia na tafakari kwa makini je dhana kama hizi zinaweza kuwa zimetengenezwa na watu waliokuwa wakitumia mawe tu katika utaalamu wa kuchonga?

Hizi ni picha mbili tofauti, Picha ya zote mbili ya upande wa kulia na kushoto zimepigwa mwaka 2011. Ya upande wa kushoto ni kutoka misitu ya Amazon, Amerika ya kusini na ya upande wa kulia ni nyumba ya Kimasai kutoka Afrika Mashariki. Je tunaweza kusema kuwa hizi ni nyumba za kipindi cha zama za mawe.


Linganisha na hii hapa chini, picha ya mwaka 2005, Jijini New York.

No comments:

Post a Comment

Qur'an 5:32