Sunday 25 March 2012

Maelezo Ya Quran Kuhusu Vilindi Vya Bahari Kuu (Qur'an And Deep Sea)



Mwenyezi Mungu Anasema ndani ya Qur'an...
Au ni kama giza katika bahari kuu, iliyo funikwa na mawimbi juu ya mawimbi, na juu yake yapo mawingu. Giza juu ya giza. Akiutoa mtu mkono wake anakaribia asiuone. Na ambaye Mwenyezi Mungu hakumjaalia kuwa na nuru hawi na nuru.
Suratun Nur 24:40

Aayah hii inataja kiza kinachopatikana katika bahari ya kina kirefu ambapo ikiwa mtu atanyoosha mkono wake, hataweza kuuona. Kiza katika bahari za kina kirefu hupatikana katika kina cha kadiri ya mita 200 na chini yake zaidi. Katika kiza hiki, hukaribia kutokuwa na mwangaza (Angalia umbo ‘A’). Chini ya kina cha mita 1000 hakuna mwangaza kabisa. [1]
Umbo 'A': Kati ya asilimia 3 na 30 ya mwangaza wa jua huakisiwa katika usawa wa bahari. Kisha, karibia rangi zote saba za spektra (mpangilio maalumu wa taswira zinazotokana na miali ya mnururisho) humezwa mmoja mmoja katika mita 200 za mwanzo, isipokuwa mwangaza wa rangi ya kibluu. (Oceans, Elder na Pernetta, uk. 27).

Wanaadamu hawawezi kuzamia zaidi ya mita arubaini bila ya msaada wa nyambizi au zana maalumu. Wanaadamu hawawezi kumudu kuishi bila ya msaada katika eneo la kina la bahari lenye kiza, kama vile kina cha mita 200.

Wanasayansi wamegundua kiza hiki hivi karibuni tu kwa msaada wa zana maalumu na nyambizi zilizowawezesha kuzamia mpaka kwenye kina cha bahari.

Pia, tunaweza kuelewa kutokana na sentesi zifuatazo za Aayah iliyotangulia kutajwa, “...katika bahari kuu, iliyofunikwa na mawimbi juu ya mawimbi, na juu yake yapo mawingu...” kuwa maji ya kina kirefu baharini hufunikwa na mawimbi ambayo juu yake kuna mawimbi mengine.
Ni wazi kuwa jozi ya pili ya mawimbi ni yaliyo katika usawa wa bahari na tunaweza kuyaona, kwani Aayah inataja kuwa juu ya mawimbi ya pili kuna mawingu. Lakini, vipi kuhusu mawimbi ya kwanza?

Wanasayansi wamegundua hivi karibuni kuwa yapo mawimbi ya ndani kwa ndani ambayo “hutokea katika eneo linalomilikiwa na misongamano baina ya mawimbi yenye tabaka zenye misongamano tofauti.” [2] (Angalia umbo ‘B’)
Umbo ‘B’: Mawimbi ya ndani kwa ndani katika eneo linalomilikiwa kati ya tabaka mbili za maji yenye misongamano tofauti. Moja ni yenye msongamano zaidi (ya chini), nyingine ina msongamano mdogo (ya juu). (Oceanography, Gross, uk. 204).

Mawimbi ya ndani kwa ndani hufunika maji ya kina kirefu cha bahari kwa sababu maji hayo ya bahari kuu yana msongamano wa juu zaidi ya maji yaliyo juu yake. Mawimbi ya ndani kwa ndani hufanya kazi kama yale ya usawa wa bahari pia yanaweza kukatika kama yafanyavyo ya usawa wa bahari. Mawimbi ya ndani kwa ndani hayawezi kuonwa na jicho la  kawaida la kibinaadamu lakini huweza kugundulika kwa kuchunguza mabadiliko ya ujoto au uchumvi katika eneo maalumu. [3]

Mwanga unapozama chini ya bahari kwa mita kumi mpaka thelathin kuelekea chini itachukua rangi NYEKUNDU, na kama mzamiaji atazama mita zaidi ya thelathini na kujikata kwa kisu basi hataweza kuiona damu yake.Kwa sababu rangi nyekundu haikuweza kufika umbali uwo wa mita thelathini.

Rangi inayofuatia ni rangi ya Chungwa yaani (Orange color). Na ukizama mita hamsini rangi inayo hakisiwa ni rangi ya Njano (Yellow).

Katika kiwango cha mita mi moja rangi ya Kijani (Green) ndio inayo hakisiwa yaani kuwa (absorbed). N akiwango cha zaidi ya mita mia mbili inapatikana rangi ya Buluu (Blue), na kuendelea…

Kwa hali hii tunaona kuwa bahari inaendelea kujiongezea kiza juu ya kiza (Progressivelly darker). Kuelekea chini, ambako nako tuna kuta mawimbi ya chini ya bahari. Kama tunavyosoma kwenye Suratun Nur 24:40 “…Mawimbi juu ya mawimbi...”

Mambo haya yanayopatikana chini ya bahari yaliginduliwa mwazoni mwa miaka ya 1900. Wataalam waligundua kuwa kuna internal waves. Ambayo yanapatikana katika layer of differential densities. Maji yaliyo chini ya bahari yana msongamano mkubwa, kuliko yalio juu yake. Mawimbi haya yaliyo chini ya maji hayawezi kuonekana kwa macho. Ila kwa kutumia vyombo maalum, ambavyo vinasoma (Dictate) halijoto (Temperature), na wingi wa munyu yaani chumvi (Salinity), katika sehemu tofauti tofauti. Na samaki wanaoishi katika kina hiki chenye kiza kinene, wanaona kwa kujitengenezea nuru mfano wa infra-red, inayotoka katika miili yao.

Wataalam wanatufahamisha kuwa kina cha mita hamsini hata nyambizi ianitaji taa kali za kuonea. Je ni nani ambaye katika karne ya kumi na nne (14C) zilizopita aliweza kuzamia na kujua kuwa chini ya bahari ni kiza na kuna mawimbi ya ndani kwa ndani!?
__
[1] Oceans, Elder na Pernetta, uk.27
[2] Oceanography, Gross, uk. 205
[3] Oceanography, Gross, uk. 205

1 comment:

  1. Allah Akbar Allah Akbar
    It's very true the quran quoted and oceanographers discovers specifically in Ocean current topics.

    ReplyDelete

Qur'an 5:32